Hasira za walimwengu dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel zinazidi
kuongezeka huku utawala huo pandikizi na ulio dhidi ya ubinaadamu
ukizidi kutengwa kimataifa. Wigo wa hasira hizo umepanuka hadi katika
nchi za Magharibi na hususan Marekani ambako viongozi wake ni waungaji
mkono wakubwa wa utawala wa Kizayuni. Wananchi wa Marekani wameshoshwa
na siasa za viongozi wao za kuoanisha manufaa ya nchi hiyo na yale ya
utawala wa Kizayuni na wamekuwa wakionyesha hasira zao kwa njia tofauti
kupinga uungaji mkono wa kibubusa wa viongozi wa Marekani kwa utawala wa
Kizayuni. Mji wa Washington huko Marekani umekuwa uwanja wa malalamiko
ya wananchi dhidi ya Israel. Wananchi wamefanya maandamano kuelekea
Ikulu ya Marekani, White House ili kuwaonesha viongozi wa nchi hiyo
upofu wa siasa zao kuhusu Israel.
Maandamano hayo yamefanyika sambamba
na sherehe za kuapishwa Barack Obama kuwa Rais wa Marekani kwa kipindi
cha pili mfululizo. Waandamanaji hao pia wametoa nara na kaulimbiu za
kuwaunga mkono Wapalestina na kutaka Marekani iache kuiunga mkono
Israel. Kitu kilichoongeza mvuto wa maandamano hayo ni kushiriki ndani
yake wazazi wa Rachel Corrie, mwanaharakati wa Kimarekani aliyeuliwa na
mabuldoza ya Israel huko Ghaza Palestina mwaka 2003. Baba wa
mwanaharakati huyo wa kike raia wa Marekani aliwahutubia waandamanaji na
kusema kuwa: Nimesimama hapa kiukumbusha serikali ya Marekani kwamba
haipaswi kuunga mkono jinai za utawala wa Kizayuni. Amesema, Wazayuni
walimuua binti yake kwa kumkanyaga kwa mabuldoza huko Ghaza miaka 10
iliyopita wakati alipokuwa anajaribu kuwazuia jinai za Wazayuni za
kuwavunjia Wapalestina nyumba zao. Kwa kweli viongozi wa Marekani wako
tayari kuuunga mkono utawala wa Kizayuni kwa thamani yoyote ile hata
kama damu za Wamarekani zitamwagika. Lakini wananchi wa Marekani
wanazidi kuamka siku baada ya siku na malalamiko yao dhidi ya siasa za
viongozi wao za kutumia mabilioni ya fedha za walipa kodi huko Marekani
kuulinda na kuundesha utawala wa Kizayuni yameongezeka sana katika miaka
ya hivi karibuni. Wazayuni wanatumia silaha za Marekani kuendeleza
jinai zao dhidi ya Wapalestina na hili nalo limekuwa likilalamikiwa
vikali na makundi yanayopinga vita nchini Marekani. Ni hivi karibuni tu
ambapo wananchi wa mji wa Seattle wa Marekani walikodi makumi ya mabasi
ya umma na kubandika matangazo yanayopinga siasa za Marekani za kutumia
fedha za wananchi wa nchi hiyo kuuendesha utawala wa Kizayuni wa Israel.
Katika siku za hivi karibuni pia, wanaharakati wa Vyuo Vikuu vya
Marekani kama vile Ridgely Fuller wamekuwa wakidhihirisha waziwazi
upinzani wao kuhusu siasa hizo za Marekani. Ukweli ni kwamba kuusaidia
kijeshi utawala wa Kizayuni wa Israel ni jambo linalopingwa na hata
sheria za Marekani kwenyewe ambazo zinapiga marufuku kutumwa misaada ya
kijeshi kwa tawala ambazo zinatumia silaha na fedha za Marekani katika
mashambulizi na ukandamizaji. Hata hivyo linapofika suala la utawala wa
Kizayuni, viongozi wa Marekani hawajali sheria zote hizo na cha ajabu ni
kuwa, utawala wa Kizayuni hautosheki na kila leo unashinikiza kupata
misaada na uungaji mkono zaidi wa viongozi wa Marekani kwa jinai zake.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment