
Mmoja wa viongozi wa jimbo hilo la Darfur Ahmad Sinin amethibitisha habari ya mateka hao na kuongeza kuwa, Sudan Kusini ni muungaji mkono nambari moja wa makundi ya waasi katika jimbo hilo. Itakumbukwa kuwa, mapigano kati ya vikosi vya serikali ya Sudan na waasi katika jimbo la Darfur yalianza mwaka 2003 ambapo mamia ya maelfu ya watu waliuawa. Nao wachambuzi wa mambo wameonya kuhusiana na njama za kujitenga kwa jimbo hilo na kuongeza kuwa, mchezo wa Sudan Kusini hautakiwi ujirejee tena nchini humo.
No comments:
Post a Comment