![]() |
Bi. Celina Kombani |
Waziri wa Sheria na Masuala ya Katiba wa Tanzania, Celina Kombani
amesema kuwa anaunga mkono tamko la Rais Jakaya Kikwete kwamba maoni ya
kuvunjwa muungano hayatapewa umuhimu na tume ya kuandaa rasimu ya katiba
mpya. Akizungumza na Radio Tehran kwa njia ya simu, Bi. Kombani amesema
mchakato wa kuvunjwa muungano ni tofauti kabisa na masuala ya katiba.
Hata hivyo Mbunge Tundu Lissu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) ambaye pia ndiye Waziri Kivuli wa Sheria na Katiba
ametofautiana na Waziri Kombani akisema kuwa Watanzania ndio wanaopaswa
kuamua iwapo wanautaka muungano uendelee kuwepo au la. Kwa upande wake
Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Wananchi CUF, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba
ametetea tamko hilo la Rais Kikwete na kuongeza kuwa muungano wa
Tanganyika na Zanzibar ni matunda ya mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka
1964. Wakizungumza kwa wakati mmoja na idhaa hii kwenye mahojiano
maalumu, watatu hao wamesema mchakato wa kutafuta katiba mpya ni zoezi
la kihistoria na wametoa wito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu na
kutoa maoni yao bila woga. Wamesisitiza kuwa Katiba mpya ndiyo chambo
pekee cha kufikia mageuzi kamili ya kisiasa, kiuchumi na kijamii.
No comments:
Post a Comment