Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 12, 2014

'Wamagharibi wabadili misimamo yao kuhusu Syria'

Rais Bashar al Assad wa Syria amesema kuwa, Wamagharibi wameanza kubadili misimamo kuhusiana na nchi yake baada ya kuelewa hatari zinazoweza kuwakumba kutokana na hatua yao ya kuwaunga mkono magaidi. Kiongozi huyo ameliambia gazeti la al-Akhbar la nchini Lebanon kuwa, viongozi wa sasa na wale wa zamani wa Marekani wamekuwa wakijaribu kuwasiliana na serikali yake lakini kutokana na lobi zinazowasukuma huko Washington, wameshindwa kueleza bayana wanachokitaka.
Matamshi ya Rais Assad yametolewa katika hali ambayo, viongozi wa kundi la G7 wamekubaliana kuweka mikakati ya kiusalama katika nchi zao ili kukabiliana na tishio la magaidi wanaotoka nchini Syria.
Inafaa kukumbusha hapa kuwa, wapiganaji wengi kwenye makundi ya kigaidi huko Syria ni raia kutoka nchi za Ulaya. Ufaransa wiki iliyopita ilitoa takwimu zinazoonyesha kuwa, kuna Wafaransa zaidi ya 900 wanaoshirikiana na makundi ya kigaidi nchini Syria.  Wakati huo huo Rais Bashar Asad amesema kamwe hatofanya mazungumzo na wapinzani wake waishio nje ya nchi na kusisitiza kuwa, mazungumzo pekee yatakayokubalika ni yale yatakayofanyika ndani ya ardhi ya Syria. Kuhusu uchaguzi uliopita wa rais kiongozi huyo amesema kuwa, Wasyria walizungumza kwa sauti kubwa na kuonyesha msimamo wao. Amesema jamii ya kimataifa inafaa iheshimu maamuzi ya Wasyria.

No comments: