Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 1, 2014

Larijani asisitiza kupambana na ugaidi Syria

Dakta Ali Larijani Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran yaani Bunge amesema kuwa, kuna ulazima wa kuendelezwa mapambano dhidi ya magaidi nchini Syria. Akizungumza kwenye kikao cha pili cha nchi marafiki wa Syria kilichofunguliwa leo mjini Tehran, Dakta Larijani ameongeza kuwa nchi za Magharibi zilifikiri kwamba, kwa kuvuruga amani na utulivu nchini Syria zingeweza kuunusuru  utawala wa Kizayuni wa Israel.
Akielezea uchaguzi wa rais ulioanza kufanyika nje ya nchi hiyo hivi karibuni, Dakta Larijani amesema kuwa, uchaguzi huo unathibitisha kwamba serikali ya Syria inafuata na kuheshimu maamuzi ya wananchi. Wakati huohuo, Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kuongezeka idadi ya nchi zinazoiunga mkono Syria kwenye mapambano dhidi ya makundi ya kigaidi, ni ishara tosha kwamba walimwengu wanahitaji amani na utulivu nchini humo. Alauddin Bourujerdi ameeleza kusikitishwa na uamuzi wa Marekani wa kutuma silaha za kisasa nchini Syria na kutoa mafunzo kwa magaidi hao na kusisitiza kwamba, jambo la kutia moyo ni kuona kwamba siku hadi siku zinaongezeka nchi zinazoiunga mkono serikali ya Syria.

No comments: