Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 1, 2014

AU kujadili kurudishiwa tena Misri unachama

Baraza la Usalama na Amani la Umoja wa Afrika linakusudia kujadili suala la kurudishiwa tena Misri uanachama katika jumuiya hiyo. Ismail al Sharqi kamishna wa baraza hilo amesema kuwa, baada ya kufanyika uchaguzi wa rais wa Misri wiki iliyopita, AU tarehe 25 Juni itafanya kikao cha kujadili juu ya kuondoa marufuku iliyowekewa Cairo katika umoja huo na kurejeshewa tena uanachama wake.

 Baada ya jeshi kumpindua Muhammad Musri rais halali wa Misri aliyechaguliwa na wananchi Julai mwaka jana, Umoja wa Afrika ulisimamisha uanachama wa Cairo katika jumuiya hiyo. Uchaguzi wa rais uliofanyika hivi karibuni ulisusiwa na mirengo mingi ya kisiasa huku watu wachache tu wakishiriki kwenye zoezi hilo.

No comments: