Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 1, 2013

Saba wauawa katika ghasia nchini Misri

Watu wasiopungua saba wameuawa katika ghasia kati ya wafuasi na wapinzani wa Rais Muhammad Mursi wa Misri. Hayo yameelezwa na duru za usalama na kitiba za nchi hiyo. Watu watano waliuawa jana katika miji ya kusini mwa Cairo, mmoja katika mji wa Beni Suef na mwingine huko Fayoum. Duru za kitiba za huko Misri zimeripoti pia kuwa watu wengine wawili walipoteza maisha wakati kulipozuka ghasia nje ya makao makuu ya Ikhwanul Muslimin katika mji mkuu Cairo. Watu zaidi ya 600 pia walijeruhiwa katika ghasia za jana.
Hayo yameripotiwa na Wizara ya Afya ya Misri. Maandamano ya jana ya kumpinga rais wa Misri yametajwa kuwa maandamano makuwba zaidi kuwahi kufanyika nchini humo katika historia ya nchi hiyo.

No comments: