Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 1, 2013

Obama: Zimbabwe ina fursa, inahitaji uchaguzi huru

Rais Barack Obama wa Marekani amesema kuwa kuboreka kwa uchumi wa Zimbabwe kunaipa nchi hiyo fursa ya kusonga mbele iwapo tu chaguzi zijazo nchini zitakuwa huru na za kiuadilifu. Obama amesema uchumi wa Zimbabwe unaanza kuimarika kwa hiyo nchi hiyo ina fursa ya kupiga hatua mbele za kimaendeleo. Rais wa Marekani aliyasema hayo jana katika hotuba yake kwa njia ya televisheni katika Chuo Kikuu cha Cape Town nchini Afrika Kusini.
Ameongeza kuwa Wazimbabwe wanaweza kujiainishia mustakbali wao bila ya kuhofia vitisho na kuadhibiwa. Rais Obama amekuwa ziarani barani Afrika ambapo hadi sasa tayari amekwishazitembelea Senegal na Afrika Kusini na mchana huu anatazamiwa kuwasili Nchini Tanzania kwa ziara ya siku mbili.

No comments: