Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, July 6, 2013

Khatami: Watawala wa Cairo wajilaumu wenyewe

Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amezungumzia hali ya sasa ya Misri na kitendo cha jeshi la nchi hiyo cha kumuondoa madarakani rais aliyechaguliwa na wananchi Muhammad Mursi na kusema, Misri ni kituo cha mwamko wa Kiislamu na kwamba wale waliopewa dhima ya kuunda serikali baada ya mapinduzi ya wananchi Waislamu walijitayarishia uwanja wa kupinduliwa na kuondolewa madarakani.

Ayatullah Ahmad Khatami amewataka wananchi wa Misri kulinda mwamko wao wa Kiislamu na wasiruhusu tena nchi hiyo kuwa mwandani wa utawala wa Kizayuni wa Israel kama ilivyokuwa serikali iliyoondolewa madarakani ya Hosni Mubarak.
Hatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran amesema kuwa, wale waliounda serikali iliyopita ya Misri awali walitoa nara za kupambana na utawala ghasibu wa Israel lakini baada ya kushika madaraka walirefusha mkataba wa Camp David na kumwita rais wa utawala ghasibu wa Israel Shimon Perez kuwa ni ndugu yao!
Ayatullah Ahmad Khatami pia ameashiria tukio la kusikitisha la kuuawa Sheikh Hassan Shehata aliyekuwa miongoni mwa maulama wa madhehebu ya Kiislamu ya Shia nchini Misri na kusema, uwahabi ambao wafuasi wake ndio waliomuua kinyama msomi huyo, ulibuniwa na Waingereza na umeendelea kuwepo kwa kutumia sera za mauaji. Amewataka maulamaa wa Kisuni kupambana na wasababishaji wa mauaji hayo na kutangaza waziwazi kwamba Uwahabi hauna uhusiano wowote na dini ya Kiislamu.

No comments: