Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

'Wapinzani Syria wasiweke sharti la mazungumzo'

Sergei Lavrov, Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa wapinzani wa Syria wanaoungwa mkono na nchi za kigeni hawapaswi kuruhusiwa kuweka masharti ili kushiriki kwenye mkutano wa pili wa Geneva. Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa suala la kutaka kumuondoa madarakani Rais Bashar Assad wa Syria halipasi kuwa sharti la wapinzani la kushiriki kwenye mazungumzo hayo ya amani.
Marekani na Russia zilikubaliana Mei 7 mwaka huu huko Moscow kuendesha mkutano wa kimataifa kuhusu Syria, ambao utaufuatia ule wa awali uliofanyika mjini Gevena mwezi Juni mwaka jana.
Muungano wa upinzani wa Syria mwezi Mei mwaka huu ulieleza kuwa hautashiriki mkutano wa pili wa Geneva iwapo haitaainishwa tarehe ya kumlazimisha Rais Bashar Assad kujiuzulu kama njia ya kutatua mgogoro wa nchi hiyo.

No comments: