Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

'Iran iko tayari kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya kieneo'

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Tehran ipo tayari kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya kieneo. Ali Akbar Salehi amesema kuhusu uamuzi wa Cairo wa kukata uhusiano wake na Syria kuwa, Misri ingeweza kuwa na nafasi kubwa katika kutafuta suluhisho la mgogoro wa nchi hiyo. Kuhusu matuiko ya Bahrain, Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran ameongeza kuwa, masuala ya Manama yanapaswa kutatuliwa na wananchi na serikali yenyewe na kwamba Tehran inaamini kuwa uingiliaji wowote nchini humo hauna faida.

Ali Akbar Salehi pia amesisitiza juu ya nafasi ya Iran katika kutatua migogoro ya kieneo na kuongeza kuwa uchaguzi wa rais wa hivi karibuni hapa nchini utaboresha uhusiano kati ya Iran na Magharibi. 

No comments: