Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

Pakistan yaitaka US ikomeshe mashambulizi ya droni

Serikali ya Pakistan imesema kuwa inataka kukomeshwa mashambulizi ya ndege za Marekani zisizo na rubani katika maeneo ya kikabila nchini humo. Sartaj Aziz, Mshauri wa Waziri Mkuu wa Pakistan katika masuala ya nje na usalama wa taifa ameliambia bunge la nchi hiyo kuwa sera mpya inabuniwa ili kukomesha mashambulizi ya ndege za Marekani zisizo na rubani nchini humo.

Aziz ameongeza kuwa serikali imeeleza wasiwasi wake kwa Washington kutokana na mashambulizi hayo na kwamba Islamabad inayachukulia mashambulizi hayo ya Marekani kuwa ni ukiukaji wa mamlaka na kujitawala nchi hiyo.

No comments: