Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 27, 2013

Mfaransa akanusha kuhisika na mauaji Rwanda

Paul Barril afisa wa zamani wa usalama wa Ufaransa amekanusha kuhusika kwenye mauaji ya halaiki ya nchini Rwanda.
Hayo yameelezwa katika hali ambayo, taasisi tatu zisizo wa kiserikali zimefungua mashtaka mahakamani zikimtuhumu afisa huyo wa Ufaransa kwa kuhusika kwenye mauaji ya kimbari nchini Rwanda.
Paul Barril mwenye umri wa miaka 67 hivi karibuni alishindwa kufika kwenye mahakama ya Marseille kutokana na hali mbaya ya kiafya, ili kujibu tuhuma za kushirikiana na genge kubwa la uhalifu nchini humo.
Muungano wa Haki za Binadamu nchini Ufaransa na Shirikisho la Kimataifa la Muungano wa Haki za Binadamu yanamtuhumu  Barril kwa kutia saini mkataba wa msaada wa kijeshi na serikali ya Rwanda wakati wa kufanyika mauaji ya kimbari nchini humo.
Inafaa kuashiria hapa kuwa, katika kipindi cha siku 100 zaidi ya watu 800,000 waliuawa kwenye mauaji ya halaiki yaliyofanywa na Wahutu wenye misimamo mikali dhidi ya Watutsi na Wahutu wenye misimamo ya wastani.

No comments: