Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

HAMAS: Ramallah ikomeshe hujuma dhidi ya raia

Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeitaka Mamlaka ya Ndani ya Palestina kukomesha hujuma zake dhidi ya wananchi wasio na hatia katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan. Afisa wa ngazi za juu katika ofisi ya kisiasa ya HAMAS, Saleh al-Aruri amesema hatua ya vyombo vya usalama vya Mamlaka ya Ndani ya Palestina ya kuwakamata raia wasio na hatia pamoja na kuwazuia shakhsia wa kisiasa ni jambo lisilokubalika na kwamba ni ukiukaji wa makubaliano ya huko nyuma kati ya makundi ya Fat'h na Hamas.
Aruri amesema kuendelea kukamatwa wanamapambano wa makundi ya muqawama ya Palestina kutaathiri makubaliano ya umoja wa kitaifa na hivyo kuzidi kumpa adui Mzayuni nguvu ya kuwagawa Wapalestina. Hii ni katika hali ambayo, siku chache zilizopita, Mamlaka ya Ndani ya Palestina ilitangaza kuwakamata wapiganaji kadhaa wa makundi ya muqawama ya Palestina baada ya msako mkali katika miji kadhaa inayodhibitiwa na mamlaka hiyo.

No comments: