Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

Boko Haram waua watu 22 Maiduguri, Nigeria

Watu 22 wameuliwa katika mashambulio tafauti yaliyofanywa na wanamgambo wa kundi la Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria. Mashambulizi hayo yaliwalenga wanafunzi na wavuvi huko Maiduguri makao makuu na mji mkubwa zaidi katika jimbo la Borno. Duru moja ya kijeshi nchini Nigeria imeripoti kuwa wanamgambo wa Boko Haram waliishambulia shule moja ya binafsi huko Jajeri katika vitongoji vya Maiduguri na kuwafyatulia risasi wanafunzi waliokuwa wakifanya mtihani wa taifa.

Wanafunzi tisa waliuliwa papo hapo huku wengine wengi wakijeruhiwa.  Mbali na wanafunzi hao, wanamgambo wa kundi la Boko Haram waliwaua pia wavuvi 13 na wachuuzi wa chai huko katika eneo la mto Alau hapo jana.  

No comments: