Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, January 26, 2013

Umoja wa Waislamu ndio ufunguo wa mafanikio yao .

Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, umoja wa Waislamu ndio utakaokuwa chimbuko la ushindi wao dhidi ya njama mbalimbali za uistikbari na maadui. Ayatullah Muhammad Kashani pia ametoa mkono wa baraka kwa kuwadia maadhimisho ya kuzaliwa mbora wa viumbe Mtukufu Mtume wa Uislamu Muhammad al Mustafa (SAW), na maadhimisho ya siku ya kuzaliwa mjukuu wa mtukufu huyo Imam Jaafar Swadiq (as) na kuanza kwa Wiki ya Umoja. Amesema kuwa, Wiki ya Umoja ni fursa muhimu ya kuimarisha umoja kati ya Waislamu wote kwa ujumla na kwamba, mambo hayo ndiyo yatakayoweza kuzishinda njama za maadui.
Akiashiria kukaribia maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya nchini Iran yaani tarehe 10 Februari, Ayatullah Muhammad Imami Kashani amesisitiza kuwa, ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, umekuwa chachu ya kupatikana heshima na maendeleo katika kila sekta nchini Iran hususan katika masuala ya sayansi na teknolojia na kuongeza kuwa, mwamko na mapambano ya wananchi wa nchi za Kiarabu dhidi ya tawala za uistikbari, nayo ni matunda ya Mapinduzi ya Kiislamu ya nchini Iran. Ameongeza kuwa, baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu hapa Iran, nchi hii imegeuka na kuwa mtetezi mkuu wa Waislamu duniani na kwamba, tofauti na misimamo hasi ya baadhi ya viongozi wa nchi za Kiarabu, Tehran imekuwa ndiyo muungaji mkono mkubwa kwa muqawama dhidi ya utawala haramu wa Kizayuni katika eneo hili.

No comments: