Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, April 22, 2012

watu watatu wauawa kwa risasi huku mtoto akiuawa kwa bomu nchini Mali

Watu watatu wameuawa kwa kupigwa risasi nchini Mali huku mtoto mdogo akiuawa kwa mripuko wa bomu kaskazini mwa nchi hiyo, hali inayoashiria kuwepo mchafukoge katika eneo ambalo linadhibitiwa kwa muda wa wiki tatu sasa na watu wenye silaha nchini humo. Aidha walioshuhudia tukio hilo wamesema kuwa, kuna uwezekano mauaji hayo yamefanywa na wezi ambao wanapatikana kwa wingi katika maeneo ya waasi wa Tuareg.
Waasi hao waliyadhibiti maeneo ya kaskazini mwa Mali baada ya kufanyika mapinduzi ya kijeshi ya tarehe 22 mwezi uliopita mwaka huu.

No comments: