
“Ni kweli kwamba tumepandisha gharama za matibabu, lakini hatuja kurupuka tu na kufanya maamuzi haya, tulikaa na bodi na kukubaliana,” alisema Almasi.Alisema hata hivyo, gharama hazikupandishwa katika maeneo yote ya tiba na kwamba zimepandishwa katika baadhi ya maeneo.
Almasi alisema sababu ya kupandishwa kwa gharama hizo ni pamoja na kupanda kwa gharama za vifaa vya kutolea huduma za matibabu.
“Taasisi hii imekuwa ikipokea asilimia 70 ya wagonjwa, wengi wao wakiwa ni majeruhi kutoka sehemu mbalimbali nchini, kwa hiyo tumefanya hivi hili kuboresha huduma za matibabu,”alisema Almasi.