Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 29, 2013

Jumamosi, Juni 29, 2013

Leo ni Jumamosi tarehe 20 Shaaban mwaka 1434 Hijria sawa na tarehe 29 Juni mwaka 2013.
Siku kama ya leo miaka 100 iliyopita Vita vya Pili vya Balkan vilianza baina ya Bulgaria na mjumuiko wa nchi za Serbia, Montenegro, Romania, Ugiriki na utawala wa Othmania. Yapata mwaka mmoja kabla katika Vita vya Kwanza vya Balkan, Bulgaria, Serbia, Ugiriki na Montenegro zilizokuwa ni sehemu ya utawala wa Othmania, zilianzisha uasi dhidi ya ufalme huo, na kutokana na kudhoofika utawala huo nchi hizo zilifanikiwa kupata uhuru. Kwa utaratibu huo karibu asilimia 80 ya ardhi zilizokuwa chini ya utawala wa Othmania barani Ulaya ikawa imeondoka katika udhibiti wa utawala huo.

Miaka 37 iliyopita katika siku kama ya leo, iliyopita Visiwa vya Ushelisheli vilivyoko  katika bara la Afrika vilipata uhuru na wananchi wa visiwa hivyo huiadhimisha siku hii ya tarehe 29 Juni kwa anuani ya Siku ya Uhuru. Hadi katikati mwa karne ya 18 ambapo Wareno walikuwa wamefanikiwa kuidhibiti ardhi ya Ushelisheli, visiwa vingi vya eneo hilo vilikuwa havijagunduliwa na hakukuwa na mtu aliyekuwa akiishi katika visiwa hivyo. Ni katika kipindi hicho, ambapo upenyaji wa Ufaransa ulipoanza. Mwishoni mwa karne ya 18 wakati harakati za mapinduzi ya Ufaransa zimepamba moto, majeshi ya Uingereza  yaliyokuwa katika moja ya maeneo ya Afrika yalivikalia kwa mabavu visiwa vya Ushelisheli.

Na siku kama ya leo miaka 1049 iliyopita kwa mujibu wa kalenda ya Hijria, Ibn Nadim mwanahistoria na mtaalamu wa masuala ya vitabu wa Kiislamu alifariki dunia. Umashuhuri wa mtafiti huyo unatokana zaidi na kitabu chake maarufu cha faharasa. Katika kitabu hicho Ibn Nadim amezitaja takriban elimu zote mashuhuri  katika ustaarabu wa Kiislamu na kisha kufafanua maisha na historia ya  wanazuoni maarufu katika elimu hizo. Kadhalika Ibn Nadim amevitaja humo vitabu na makala zilizoandikwa kuhusiana na elimu hizo.

No comments: