Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, September 23, 2012

Uamuzi wa Marekani wa kulifuta jina la kundi la Munafiqin katika orodha ya makundi ya kigaidi

Vyombo vya habari vimeripoti kuwa serikali ya Marekani imeamua kuliondoa jina la kundi la kigaidi la Munafiqin MKO katika orodha ya makundi ya kigaidi. Kanali ya habari ya BBC imelinukuu shirika la habari la Reuters na kutangaza kuwa serikali ya Marekani imeamua kuliondoa jina la kundi la kigaidi la Munafiqin MKO katika orodha rasmi ya makundi ya kigaidi. Shirika hilo la habari limewanukuu viongozi rasmi wawili wa Marekani kwa sharti la kutotajwa majina yao wakisema kuwa serikali ya Washington imeamua kulifuta rasmi jina la kundi la kigaidi la Munafiqin katika orodha ya makundi ya kigaidi ifikapo tarehe Mosi mwezi Oktoba mwaka huu.
Kuhusiana na habari hiyo kumeashiriwa nukta hii kwamba Hillary Clinton Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani ametoa uamuzi wa mwisho juu ya suala hilo. Marekani imeamua kulifuta jina la kundi la kigaidi la Munafiqin yaani MKO katika orodha ya makundi ya kigaidi kwa kisingizio cha kufungwa kambi ya Ashraf huko katika mkoa wa Diyala nchini Iraq na kupigwa marufuku vitendo vya kigaidi vya kundi hilo tangu mwaka 2003. Kwa mujibu wa makubaliano yaliyosainiwa mwezi Disemba mwaka jana kati ya serikali ya Iraq na kundi la kigaidi la Munafiqin, wanachama wa kundi hilo wanapaswa kuhamishiwa polepole katika kambi ya Liberti na baada ya kufika hapo mazingira yaweze kuandaliwa kwa ajili ya kuhamishwa tena wanachama hao na kupelekwa katika nchi nyingine. Hii ni katika hali ambayo oparesheni ya kuwahamishia wanachama wa kundi la kigaidi la Munafiqin katika kambi ya Liberti huko Baghdad imekamilika. Kambi ya Liberti ilikuwa kambi kubwa zaidi ya Marekani huko Iraq ambayo imekuwa ikitumiwa kwa muda na wanachama wa kundi la kigaidi la Munafiqin baada ya vikosi vamizi vya Marekani kuondoka huko Iraq mwishoni mwa mwaka jana. Jambo lililo wazi na lisiloweza kukanushika hapa ni kuwa serikali ya Marekani inatumia maana ya neno 'mapambano dhidi ya ugaidi' kwa maslahi yake katika kupambana na kundi la kigaidi la Munafiqin.  Njia inayotumiwa na serikali ya Marekani katika kuamiliana na kundi hilo la kigaidi ni uthibitisho kamili wa maana ya ugaidi na migawiko yake yaani ugaidi mzuri na mbaya kwa mtazamo wa viongozi wa Washington. Radiamali  ya serikali ya Marekani  kwa vitendo vya kigaidi vilivyofanywa na kundi la Munafiqin nchini Iran ambalo limewaua Wairani elfu 12 inapaswa kuzingatiwa katika fremu ya  migawiko ya ugaidi kwa mujibu wa  wa serikali ya Marekani yaani ugaidi mzuri na ugaidi mbaya. Marekani na waitifaki wake wa Ulaya wamezusha chuki na uadui dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutokana na kusimama kwake imara mbele ya siasa za mabavu na za kupenda kujitanua za nchi hizo. Kwa mtazamo wa nchi hizo za Magharibi harakati yoyote iliyo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ikiwemo hata vitendo vitakavyosababisha kuuliwa shahidi wanaume, wanawake na watoto wa Iran   ni halali.
Kufungwa kambi ya Ashraf hakuwezi kuhalalisha kivyovyote kufutwa jina la kundi la kigaidi lililokuwa limewekwa katika faharasa ya makundi ya kigaidi. Yoyote aliyehusika kumwaga damu za maelfu ya watu wasio na hatia anapasa kushtakiwa na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria. Hata hivyo serikali ya Marekani inafanya kila iwezalo ili kuzuia kusambaratika kundi la Munafiqin la MKO ili kwa njia hiyo iweze kulitumia tena kundi hilo katika vitendo vyake vya kuingilia masuala ya hapa nchini na ya nchi nyingine za eneo. Kusalia au kufutwa jina la kundi la Munafiqin katika orodha ya makundi ya kigaidi hakuwezi kubadilisha kivyovyote vile sura chafu ya kundi hilo.  Serikali ya Marekani imeamua kulifuta jina la kundi la kigaidi la Munafiqin katika faharasa ya makundi ya kigaidi ili kuhalalisha uungaji mkono wake kwa kundi hilo chini ya mwavuli wa hatua za kibinadamu.

No comments: