Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 1, 2012

Waindonesia wapata kisanduku cheusi cha ndege ya Russia ‘iliyoangushwa na Marekani’

Wanakijiji wa Indonesia wamepata kisanduku cheusi cha ndege ya abiria ya Russia aina ya Sukhoi Superjet 100 ambayo Russia inasema iliangushwa na Marekani kusini magharibi mwa Indonesia mapema mwezi Mei.
Kitengo cha kiintelijensia cha jeshi la Russia GRU kimesema kuwa ndege hiyo ya abiria iliyosababisha vifo vya watu 45 iliangushwa kwa maksudi na Marekani ili kurudisha nyuma jitihada za Moscow za kutawala biashara ya usafiri wa anga katika eneo la Asia na Pasifiki. Ndege hiyo ambayo ni ya kisasa ilikuwa katika safari ya majaribio wakati ilipoanguka Mei 9 nchini Indonesia.
Maafisa wa usalama Russia wamesema kwa muda mrefu wamekuwa wakichunguza harakati za wataalamu wa masuala ya elektroniki wa jeshi la Marekani walio na kituo chao katika uwanja wa ndege wa Jakarta, Indonesia.

No comments: