Umoja wa Ulaya umeukosoa vikali utawala haramu wa Israel kutokana na kile ulichokiita ni utawala huo kuendeleza ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi katika ardhi za Palestina unazo zikalia kwa mabavu.
Mawaziri hao wa Mambo ya Nje wa Ulaya wameyasema hayo hii leo katika ripoti ya matamshi makali kwamba, utawala huo wa Israel unavunja mpango wa amani kwa kuendeleza ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi.
Mawaziri hao wa Mambo ya Nje wa Ulaya wameyasema hayo hii leo katika ripoti ya matamshi makali kwamba, utawala huo wa Israel unavunja mpango wa amani kwa kuendeleza ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kiyahudi.
Ripoti hiyo aidha umeutaka utawala huo ghasibu kusimamisha mara moja ujenzi huo usio wa kisheria kwenye ardhi zinazokaliwa kwa mabavu, sambamba na kubadilisha muamala mbaya unaoufanya utawala huo dhidi ya Wapalestina. Ripoti hiyo yenye kurasa tatu ya Mawaziri hao wa Umoja wa Ulaya imeongeza kuwa, ujenzi huo unapingana kabisa na sheria za Umoja wa Mataifa.
No comments:
Post a Comment