Vikosi vya usalama vya serikali ya mpito ya Misri inayoungwa
mkono na jeshi vimewashambulia wanafunzi waliokuwa wanaandamana katika
eneo la bweni katika Chuo Kikuu cha Al Azhar mjini Cairo. Katika
patashika hiyo wanafunzi kadhaa wa chuo kikuu hicho wamejeruhiwa baada
ya askari usalama kutumia risasi bandia na gesi ya kutoa machozi katika
ghasia hizo. Tangu jeshi lilipopindua serikali iliyochaguliwa na
wananchi ya Rais Mohamed Mursi mwaka uliopita Chuo Kikuu hicho cha Misri
kimekuwa uwanja wa mapambano kati ya askari usalama na wanafunzi.
Itakumbukwa kuwa, Mei 11 mwaka huu korti ya wilaya ya Nasr mjini
Cairo iliwahukumu kifungo cha miaka minne jela wanafunzi 36 wa Chuo
Kikuu cha Al Azhar huku kila mmoja akipigwa faini ya dola 4,300.







No comments:
Post a Comment