Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, May 14, 2014

IGAD: Pande za S. Kusini ziheshimu makubiliano

Jumuiya ya kieneo ya Mashariki mwa Afrika IGAD imesisitiza udharura wa kuheshimiwa makubaliano ya usitishaji vita nchini Sudan Kusini. Seyoum Mesfin mpatanishi  wa IGAD katika mgogoro wa Sudan Kusini amesema, pande mbili zinapaswa kuendeleza mazungumzo na kusitisha vita sambamba na kujitahidi kutafuta suluhu ya kisiasa katika nchi hiyo ya mashariki mwa Afrika. Kutokana na mashinikizo ya kimataifa vikosi vya serikali ya Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini na wanamgambo watiifu kwa kiongozi wa waasi Riek Machar siku kadhaa zilizopita walilazimika kutia saini makubaliano ya amani mjini Addis Abbas Ethiopia, lakini bado vipengee vya makubaliano hayo havijatekelezwa ipasavyo.
Hayo yanaripotiwa huku Ban Ki Moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akitaka kuundwa mahakama maalumu kwa ajili ya kuwahukumu waliotenda jinai dhidi ya binadamu nchini Sudan Kusini.  

No comments: