Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, May 14, 2014

Uingereza yampatia kinga ya kidiplomasia Tzipi Livni

Serikali ya Uingereza imempatia kinga ya kidiplomasia Waziri wa Sheria wa utawala wa Kizayuni wa Israel Tzipi Livni, ili kuzuia asikamatwe atakapoitembelea nchi hiyo kutokana na jinai dhidi ya binadamu zinazomkabili.  Mwaka 2009 mahakama ya Uingereza ilitoa hukumu ya kukamatwa Livni kutokana na kuwa mjumbe wa Baraza la Mawaziri la Israel lililoratibu kuuawa zaidi ya Wapalestina 1,400 katika Ukanda wa Gaza kati ya Disemba 2008 hadi Januari 2009.  Mwaka huo Livni alilazimika kuvunja safari yake ya kutembelea Uingereza.
 Hata hivyo Ofisi ya Jumuiya ya Madola na Masuala ya Nje ya Uingereza (FCO) imetangaza kuwa, eti imempa 'hadhi ya kutekeleza jukumu maalumu' Tzipi Livni ambaye anatarajiwa kutembelea London wiki ijayo.  Hatua hiyo imekosolewa na Kituo cha Kutetea Haki za Binadamu cha Palestina huko Gaza.

No comments: