Syria imeutuhumu utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa unawaunga
mkono wanamgambo wanaopigana dhidi ya serikali ya Rais Bashar la Assad
wa nchi hiyo. Bashar Ja'afari Mwakilishi wa Syria katika Umoja wa
Mataifa amesema kuwa, Israel inasaidia makundi ya kigaidi katika
mapigano hayo na kwamba Tel Aviv imemfadhili, kumpa mafunzo na hifadhi
kamanda mpya wa kundi linalojiita Jeshi la Ukombozi wa Syria (FSA).
Aidha Mwakilishi wa Syria katika moja wa Mataifa ameikosoa Marekani
na washirika wake kwa kuingilia masuala ya ndani ya Syria na kuendelea
kuuunga mkono makundi ya kitakfiri ndani ya nchi hiyo ya Kiarabu.
Mwezi Februari kamanda mmoja wa Israel alikiri kwamba jeshi la
utawala huo ghasibu linashirikiana na wanamgambo wanaopigana dhidi ya
serikali ya Damascus. Pia ripoti zimeeleza kuwa, mamia ya waasi
wanaopigana Syria hupatiwa matibabu katika hospitali za Israel.







No comments:
Post a Comment