Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, May 21, 2014

Mkutano wa Iran na IAEA wamalizika mjini Tehran

Mkutano kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) umemalizika hapa mjini Tehran huku pande mbili hizo zikielezea kufurahishwa na anga ya kirafiki ya mkutano huo. Ujumbe wa IAEA ulikutana na maafisa wa ngazi za juu wa serikali ya Iran jana Jumanne na kufanya mazungumzo ya kina kuhusiana na miradi ya nyuklia ya hapa nchini yenye malengo ya amani. Ingawa taarifa rasmi ya mkutano huo haijatolewa lakini baadhi ya wajumbe na wanadiplomasia waliohudhuria kikao hicho wamesema majadiliano yalikuwa ya kina na anga ya kirafiki ilitanda katika kipindi chote cha mkutano.
IAEA na Iran zimekubaliana kuendeleza mazungumzo katika siku za usoni ili kuongeza zaidi kasi ya ushirikiano wa pande mbili. Mkutano huo umefanyika siku chache kabla ya kutolewa ripoti ya wakala huo wiki hii. Ripoti hiyo itajadiliwa baadaye mwezi ujao kwenye mkutano wa Bodi ya Magavana wa IAEA.

No comments: