Umoja wa Afrika umezitaka pande zote za Sudan kuitikia wito wa
mazungumzo ya kitaifa. Nkosazana Dlamin Zuma Mkuu wa Kamisheni ya Umoja
wa Afrika amesisitiza umuhimu wa mazungumzo ya kitaifa ya Sudan kwa
ajili ya mutakbali wa nchi hiyo na kuzitaka pande zote za nchi hiyo
kutopoteza fursa ya mazungumzo hayo. Katika taarifa iliyotolewa na Umoja
wa Afrika, Zuma amesema AU inatiwa wasiwasi na mabadiliko yanayojiri
nchini Sudan kwani mabadiliko hayo yanaweza kuwa na taathira hasi kwa
mwenendo wa mazungumzo ya kitaifa.
Mkuu wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika
amesisitiza kuwa AU inashikamana na ahadi yake ya kuisaidia Sudan
kufanikisha mazungumzo hayo ya kitaifa.
Mwezi Januari Rais Omar al Bashir wa Sudan alitoa pendekezo la
kufanyika mazungumzo ya maridhiano ya kitaifa na makundi na vyama vya
upinzani na pia harakati za waasi kama njia ya kutatua mgogoro wa nchi
hiyo.







No comments:
Post a Comment