Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, May 21, 2014

AI yalaani ukiukaji wa haki za binadamu nchini Bahrain

Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limelaani ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Bahrain sambamba na kukosoa mwendo wa kobe wa serikali katika kufanya mageuzi katika idara ya mahakama. Shirika hilo limesema kwenye ripoti yake kwamba, utawala wa Aal Khalifa umeshindwa kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya maafisa wake waliotenda jinai dhidi ya binadamu; jambo linalokiuka sheria za kimataifa. Ripoti hiyo ya Amnesty International inafuatia uchunguzi wa kina wa shirika hilo wakati wa ziara yake nchini Bahrain.
Maafisa wa AI walikuwa Bahrain kati ya Mei 3 hadi 9 ambapo walikutana na watu mbalimbali wakiwemo wafungwa wa kawaida na wale wa kisiasa.
Taarifa ya Amnesty International imeitaka serikali ya Manama kuchukua hatua za dharura kulinda uhuru wa kujieleza na kukutana wa raia wa nchi hiyo.  

No comments: