Maafisa wa Afya wa Saudi
Arabia wametangaza kuwa idadi ya watu waliopoteza maisha yao kutokana na
virusi vinavyoshambulia mfumo wa kupumua vya coronavirus au MERS
imefikia 160, ikiwa ni baada ya kufariki dunia watu watatu hapo jana.
Wizara ya Afya ya Saudia imesema kuwa, vifo hivyo vimetokea katika mji
mkuu Riyadh, na miji ya magharibi ya Jeddah na Madina.
Ripoti zinaonesha kuwa, tangu
virusi hivyo vilipoguduliwa nchini humo hadi sasa watu karibu 500
wameambukizwa ugonjwa huo. MERS ni virusi vya kundi la Coronavirus
vinavyojumuisha vimelea vinavyosababisha mafua au matatizo katika mfumo
wa kupumua. Virusi hivyo husababisha maambukizi kwenye mapafu, ambapo
mgonjwa hukohoa, hushindwa kupumua na husumbuliwa na homa.







No comments:
Post a Comment