Habari kutoka Nairobi, Kenya, zinasema kuwa watu takribani 13
wamepoteza maisha na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa kufuatia miripuko
iliyotokea leo alasiri katika eneo la Gikombaa karibu na kituo kikuu cha
mabasi ya mikoani. Mashuhuda wamesema mripuko wa kwanza umetokea ndani
ya daladala na mwingine ukatokea muda mfupi baadaye karibu na soko kuu
la Gikombaa. Msemaji wa Polisi, Bi Gatiria Mboroki amesema uchunguzi
umeanzishwa na kwamba tayari washukiwa wawili wametiwa mbaroni.
Wakati huo huo Rais Uhuru Kenyatta ametoa mkono wa pole kwa familia
zilizopoteza wapendwa wao. Rais Kenyatta amesema Kenya inapitia kipindi
kigumu katika masuala ya usalama na ametoa mwito kwa Wakenya
kushirikiana na vyombo vya usalama katika kukabiliana na vitendo vya
ukosefu wa usalama. Kiongozi huyo amekosoa nchi za Magharibi ambazo
zimewataka raia wao wasiitembelee Kenya akisema nchi hizo si marafiki wa
dhati kwani badala ya kuisaidia nchi yake kukabiliana na ugaidi,
zimeamua kutoa onyo kwa raia wao lengo kuu likiwa ni kulemaza sekta ya
utalii nchini Kenya.







No comments:
Post a Comment