Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetangaza kuwa, tarehe ya
kuanza kesi dhidi ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta imesukumwa mbele hadi
Novemba 12, mwaka huu.
Hatua hiyo inakusudiwa kuwawezesha mawakili wake kujiandaa
barabara.Awali, ICC ilikuwa imepanga kesi hiyo ianze kusikizwa Julai 9,
ingawa Bw Kenyatta, kupitia wakili wake, aliomba kuongezewa muda wa
kujitayarisha kutokana na kuchelewa kwa upande wa mashtaka kueleza
ushahidi unaotumiwa dhidi yake.
Taarifa iliyotolewa na mahakama hiyo
imesema tarehe hiyo mpya imezingatia ombi la mtuhumiwa pamoja na masuala
mengine muhimu.
Rais wa Kenya anakabiliwa na makosa matano ya jinai dhidi ya binadamu
ambayo ni mauaji, uhamishaji wa watu kwa lazima, ubakaji, dhulma na
vitendo vya kinyama wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007.
No comments:
Post a Comment