Tido, akiwa bado anaishi nchini Kenya, na baada ya kuwa
mwandishi wa habari wa kwanza kutangaza kuuawa kinyama kwa aliyekuwa
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Kenya, Dr. Robert Ouko, aliamua
kuchukua nafasi ya mwaliko aliopatiwa na BBC kwenda London kwa ziara ya
mafunzo ya miezi mitatu. Akiwa kwenye maandalizi ya safari hiyo, alienda
kwanza Dar es Salaam kuaga wazazi. Huku nyuma, maafisa wa Usalama wa
Serikali ya Kenya walienda kumtafuta ofisini kwake mjini Nairobi kwa nia
ya kumkamata. Sasa endelea…
Wafanyikazi wa ofisi za jirani na ile ya VOA niliyokuwa nikifanyia kazi pale Chester House, Nairobi, na wao hawakujua nilipokuwa, kwani niliondoka bila ya kuwaaga.
Wafanyikazi wa ofisi za jirani na ile ya VOA niliyokuwa nikifanyia kazi pale Chester House, Nairobi, na wao hawakujua nilipokuwa, kwani niliondoka bila ya kuwaaga.
Halikadhalika, wale wafanyikazi wengine wote
niliokuwa nikifanya kazi nao ofisi moja walikuwa kwenye likizo zao,
hivyo ofisi za VOA zilikuwa zimefungwa. Kwahiyo, hao jirani zangu wakawa
wanatapatapa kutafuta njia ya “kunitonya” kwamba nisiende ofisini maana
natafutwa.
Wakiwa kwenye lindi la mtihani huo, mmoja wao
akamkumbuka rafiki yangu mkubwa ambaye alikuwa na tabia ya kunitemebelea
pale ofisini mara kwa mara. Yeye na wenzie wakaona kwamba huyo lazima
angejua pale nilipo, hivyo wakamtafuta na kumfahamisha hali ya mambo.
Ilikuwa majira ya saa tano mchana hivi wakati
nilipowasili nyumbani kwa wazee wangu Chang’ombe. Wakati bado
tunajuliana hali, ghafla nikaambiwa kuna simu inayonitafuta. Nikashangaa
huku najiuliza: ni nani huyo ambaye mara hii keshafahamu kwamba
nimewasili Dar?Nikaambiwa alikuwa ni rafiki yangu wa Nairobi,
Livingstone Amaumo. Nikashangaa zaidi.
Livingstone alikuwa rafiki yangu mkubwa sana kwa kipindi chote nilichokuwepo nchini Kenya. Yeye alikuwa meneja kwenye kampuni kubwa ya kimataifa ya kurikodi na kuuza nyimbo, CBS.
Livingstone alikuwa rafiki yangu mkubwa sana kwa kipindi chote nilichokuwepo nchini Kenya. Yeye alikuwa meneja kwenye kampuni kubwa ya kimataifa ya kurikodi na kuuza nyimbo, CBS.
Wakati ule ni nyimbo za sahani za santuri. Alikuwa
mtu mpole sana, mnyenyekevu mno, mkarimu kupita kiasi. Muungwana kweli
kweli. Akipenda sana muziki wa Kitanzania.
Kwakuwa nilikuwa nafahamiana na wanamuziki maarufu
karibu wote Watanzania wakati huo, wakina: Muhidini Gurumo, Hassan
Bitchuka, Ndala Kasheba, Kiki, Maneti, Juma Kilaza, Nguza Viking,Cosmas
Tobias Chidumule, Marijani Shabani, Chinyama Chiaza aliyekuwa kiongozi
wa Orchestra Maquisdu Zaire nyakati hizo, Patrick Balisidya wa Afro 70
Band, na wengine wengi, nilimunganisha nao.
Wakati mmoja tuliwachukua baadhi ya wanamuziki wa
kikundi cha Mlimani Park Orchestra, kikiwa bado kipya siku hizo, wakaja
Nairobi kurikodi nyimbo kadhaa, ndipo wimbo wao wa “Nawashukuru Wazazi”
ukavuma sana sana nchini Kenya.
Kwakweli Livingstone alikuwa zaidi ya rafiki.
Alikuwa ni kama ndugu yangu wa Kikenya. Aliwafahamu ndugu zangu wote na
jamaa zangu kadhaa. Alipenda sana kuja kutembea Tanzania.Aidha,
hakuupenda tu muziki wa Kitanzania bali pia aliipenda sana Tanzania kwa
ujumla wake hata wakati mkewe alipojifungua mtoto wao wanne wa kiume na
wamwisho, wakamuita Nyerere.
Nikachukua simu ya Livingstone na kauli yake ya
kwanza kabisa ikawa:“Namshukuru Mwenyezi Mungu kwamba upo huko.”
Nikamwuliza, “Kwani kuna nini?” Ndipo alipoponifahamisha kisanga kile
cha mimi kutafutwa na jamaa wa usalama. Nikapigwa na ganzi.
Kwa muda mfupi uliofuata nikawa natafakari hili na
lile. Nikajisemea kimoyomoyo: “Hawa jamaa wananitafutia nini? Wanataka
tu kunitia matatani bila ya sababu yoyote ya maana? “Wanataka tu
kuniharibia maisha yangu na ya watoto wangu waliokuwa wadogo bado!”
Watoto wetu tuliwaacha pekee yao Nairobi kwani
tulikuwa tumepanga kurejea huku baada ya muda mfupi tu. Niliamua
kujinyamazia, bila ya kumwambia na kumtia taharuki, Mwangaza, mke wangu.
Lakini wakati nikiendeleakuwaza na kuwazua, simu
ya pale nyumbani ikalia kwa mara nyingine. Nikaambiwa tena ilikuwa simu
yangu. Nikadhani labda ni Livingstone yule rafiki yangu, labda kasahau
jambo. Lakini nilipoichukua ikawa ni simu kutoka ubalozi wa Marikani,
Nairobi.
No comments:
Post a Comment