Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 17, 2014

Mpatanishi wa Umoja wa Afrika awasili nchini Sudan

Thabo Mbeki, mpatanishi wa Umoja wa Afrika katika mazungumzo ya kitaifa ya Sudan leo amewasili mjini Khartoum, kwa lengo la kufatilia mwenendo wa mazungumzo hayo yaliyopendekezwa na Rais Omar al Bashir wa nchi hiyo. Mbeki anatazamiwa kuzungumza na kubadilishana mawazo kuhusu mazungumzo ya kitaifa na viongozi wa vyama na makundi ya upinzani wakiwemo wa chama cha Umma, chama cha Kongresi ya wananchi, chama cha Muungano wa Kidemokrasia na chama cha Mageuzi Sasa.
Mahmoud Kan, mwakilishi wa Umoja wa Afrika nchini Sudan amesema, kutokana na ombi la serikali ya Khartoum na pande nyengine nchini humo, Mbeki atajaribu kuzikurubisha pande husika katika mazungumzo hayo ya kitaifa na kujenga hali ya kuaminiana baina yao pasina kuingilia mchakato wa mazungumzo hayo. Akiashiria mazungumzo ya Addis Ababa baina ya serikali ya Sudan na makundi ya waasi, mwakilishi wa AU nchini humo amesema mazungumzo hayo yataanza tena katika wiki ya mwisho ya mwezi huu wa Mei. Mnamo mwezi Januari mwaka huu Rais Omar al Bashir wa Sudan alitangaza mpango wa mazungumzo ya kitaifa kati ya serikali na makundi na vyama vya siasa pamoja na waasi wanaotumia silaha kama njia ya kumaliza mgogoro ulioikumba nchi hiyo

No comments: