Wanajeshi wanane kutoka Chad wanaolinda amani katika Jamhuri ya Afrika
ya Kati wameuawa nchini humo. Msemaji wa vikosi vya kulinda amani vya
Kiafrika katika Jamhuri ya Afrika ya Kati MISCA amesema kuwa, wanajeshi
hao wameuawa kwenye mapigano yaliyojiri Bangui, mji mkuu wa nchi hiyo.
Hata hivyo, msemaji huyo wa MISCA hakutoa maelezo zaidi kuhusiana na
tukio hilo.
Hivi karibuni, vikosi vya MISCA vilipanga mkakati wa
kuwaondoa wanajeshi wa Chad katika mji mkuu wa Bangui na kuwapeleka
kaskazini mwa nchi hiyo kwa lengo la kulinda amani. Inadaiwa kuwa, Chad
inawaunga mkono wafuasi wa waasi wa zamani wa Muungano wa Seleka ambao
ni Waislamu. Inafaa kuashiria hapa kuwa, jana wafuasi wa kundi la Anti
Balaka walitekeleza mauaji ya kinyama kwenye Masjidul Nour mjini Bangui
kwa kuwauwa Waislamu wasiopungua 23 wakiwemo wanawake na watoto.
Waislamu hao walikimbilia Msikitini ili kupata hifadhi, lakini
hawakusalimika kwani walivamiwa na Wakristo wa kundi la Anti Balaka na
kuuawa kwa kukatwakatwa kwa mapanga na mundu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment