Wahudumu wa shirika la utoaji
misaada la Msalaba Mwekundu wamekusanya miili 44 katika barabara za mji
mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati Bangui, ikiwa ni baada ya mapigano
makali yaliyojiri kwa siku mbili zilizopita. Georgios Georgantas, mkuu
wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu amesema, kuna uwezekano miili
hiyo ni sehemu tu ya idadi kubwa ya watu waliouawa katika mapigano
yanayoendelea kwenye mji huo. Waasi wa zamani wa Seleka ambao wengi wao
ni Waislamu wamekuwa wakipambana na wanamgambo wa Kikiristo kwa siku
kadhaa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Hayo yanajiri huku askari 6 wa
kulinda amani wa Chad wakiuawa pia katika nchi hiyo, na kugunduliwa pia
kaburi la umati lililokuwa na miili ya watu 30 karibu na kituo kimoja
cha jeshi.
Wakati huo huo viongozi wa dini za
Kiislamu na Kikristo katika Jamhuri ya Afrika ya Kati wameutaka Umoja wa
Mataifa kupeleka askari wa kulinda amani nchini humo ili kuhitimisha
mapigano.







No comments:
Post a Comment