Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 7, 2013

Mawaziri wa maji wa nchi za Kiarabu wakutana Cairo

Kikao cha Tano cha Mawaziri wa Maji wa Nchi za Kiarabu, kimefanyika mjini Cairo Misri, kwa minajili ya kujadili tatizo la kupungua maji katika nchi hizo. Kikao hicho kimefanyika katika ofisi za Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) mjini humo. Akizungumza katika kikao hicho, Nabil al Arabi Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amesema kuwa, kuna changamoto nyingi mbalimbali zinazozikabili nchi wanachama, kuhusiana na uga wa kuhifadhi maji yanayohitajiwa na nchi za hizo za Kiarabu, hasa kwa kuzingatia mabadiliko ya hali ya hewa na ukame wa muda mrefu katika baadhi ya nchi hizo. Nabil al Arabi amesisitizia udharura wa kuwepo mashirikiano makubwa kati ya nchi za Kiarabu,
kwa ajili ya kutatua migogoro inayotokana na ukosefu wa maji na ukame. Ameongeza kuwa, suala la kudhamini maji ni miongoni mwa masuala muhimu ya maisha na kuzitaka nchi hizo kuimarisha mashirikiano. Hatua hiyo, inakuja ikiwa ni baada ya kujiri suutafahumu kati ya nchi za Misri na Ethiopia kuhusiana na matumizi ya maji ya Mto Nile. Wakati huo huo Mshauri wa Rais wa Misri wa masuala ya kisiasa amesema kuwa, nchi hiyo itaitaka Ethiopia kuacha kujenga bwawa katika mto wa Blue Nile, na kuongeza kuwa, Misri ina hofu kuwa ujenzi huo utapunguza fungu lake la maji kutoka mto huo.

No comments: