Baraza la Mawaziri nchini Madagascar, limekubaliana kusogeza mbele
uchaguzi wa rais wa nchi hiyo, hadi mwezi Agosti mwaka huu. Waziri wa
Mawasiliano wa Madagascar Harry Laurent Rahajason ametangaza leo kuwa,
Baraza la Mawaziri limekubaliana kuwa, uchaguzi wa rais uliokuwa
umepangwa kufanyika tarehe 24 Julai, utafanyika tarehe 23 mwezi Agosti
mwaka huu. Kiongozi huyo wa Madagascar amefafanua kuwa, ili kuiepusha
nchi hiyo na mgogoro wa kisiasa unaoikabili hivi sasa Madagascar, lazima
tarehe hiyo iungwe mkono pia na Tume ya Uchaguzi ya nchi hiyo na Umoja
wa Mataifa. Hatua hiyo inatajwa kuwa ni kuitikia ombi la mahakama
maalumu ya uchaguzi nchini humo CES ambayo tarehe 28 mwezi jana, ilitaka
kufanyiwa uchunguzi wa haraka nukta mbili za kusimamishwa msaada wa
fedha za bajeti ya uchaguzi na kadhia ya kupingwa na jumuiya ya
kimataifa, ugombea wa wagombea watatu wa nchi hiyo. Hii ni katika hali
ambayo hapo jana mahakama ya uchaguzi ya nchi hiyo, iliidhinisha
wagombea hao watatu ambao ni pamoja na Rais Andry Rajoelina, Lalao
Ravalomanana, mke wa Marc Ravolamanana rais wa zamani wa Madagascar na
Didier Ratsiraka dikteta wa zamani wa nchi hiyo kushiriki katika
uchaguzi huo wa rais nchini humo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)






No comments:
Post a Comment