Serikali ya Saudi Arabia imeendeleza chuki na uadui wake dhidi ya
serikali ya Syria, baada ya kuutaka Umoja wa Ulaya kutekeleza kivitendo
uamuzi wake wa kuyaondolea vikwazo makundi ya kigaidi nchini Syria.
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Saudi Arabia Saud al Faisal
amesisitiza kuwa, Umoja wa Ulaya unapasa kutekeleza kivitendo maamuzi
iliyoyachukua ya kuyaondolea vikwazo vya silaha makundi ya kigaidi
yanayopambana na majeshi ya Syria.
Al Faisal amesisitiza pia ulazima wa
kuchukuliwa misimamo ya kimataifa ya kukabiliana na waungaji mkono wa
serikali ya Syria na kusema kuwa, baadhi ya duru za kimataifa zinatoa
visingizio juu ya uungaji mkono wao kwa makundi ya kigaidi nchini Syria
na kubainisha kuwa tatizo kuu ni hitilafu zilizopo kati ya wajumbe wa
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusiana na mgogoro wa Syria.
Serikali ya Rais Bashar al Assad wa Syria imekuwa ikikabiliwa na
machafuko kutokana na misimamo yake madhubuti ya kuwaunga mkono wananchi
wa Palestina na kuwa dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.







No comments:
Post a Comment