Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 1, 2013

Wamagharibi wasababisha hasara ya mabilioni Syria

Waziri mmoja wa Syria amesema kuwa ugaidi wa zaidi ya miaka miwili unaofadhiliwa na nchi za Magharibi huko Syria umeharibu majengo ya serikali yasiyopungua 9000 na kuisababishia setka ya umma hasara ya dola bilioni 15. Omar Al Ibrahim Ghalaounji Waziri wa Serikali za Mitaa wa Syria amesema hasara za mabilioni hayo ya dola zilisababishwa na magaidi kati ya mwezi Machi mwaka juzi na Machi mwaka huu.

Omar al Ghalaounji amesema hasara zote hizo ni matokeo ya mashambulizi ya kigaidi dhidi ya majengo ya serikali na miundo mbinu ya Syria.
Hii ni katika hali ambayo Abdullah al Dardari Waziri wa zamani wa Mipango wa Syria pia hivi karibuni alieleza kuwa mgogoro wa nchi hiyo umeisababishia nchi hiyo hasara ya kati ya dola bilioni 60 hadi 80.

No comments: