Umoja wa Mataifa umeanza operesheni ya kulinda amani nchini Mali
kwa kuanza kusimamia askari 6,000 wa nchi za Afrika magharibi ambao
tayari wapo nchini humo.
Hafla za kuanza operesheni hizo zimefanyika leo mjini Bamako.
Imepangwa kuwa hadi ifikapo mwezi Disemba kikosi cha kulinda amani cha
UN nchini Mali kitakamilika kwa kuwa na askari 12,640. Kikosi hicho
kipya kinaaza shughuli zake ikiwa miezi kadhaa imepita tangu Ufaransa
iliyoishambulia kijeshi nchi hiyo kwa kisingizio cha kupambana na waasi,
ianze kuondoa wanajeshi wake nchini Mali.
Kikosi hicho kinachojulikana
kama MINUSMA kitaongozwa na jenerali Jean-Bosco Mazura wa Rwanda ambaye
alikuwa afisa msaidizi wa kikosi cha askari wa Afrika wa kusimamia amani
katika jimbo la Magharibi mwa Sudan la Darfur.
Operesheni hizo zina lengo la kuimarisha amani katika nchi hiyo ya
magharibi mwa Afrika kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu mwishoni mwa mwezi
huu.







No comments:
Post a Comment