Russia imeitaka Marekani kuweka wazi msimamo wake kuhusu mkutano
wa Geneva 2 utakaofanyika kwa lengo la kuutafutia ufumbuzi mgogoro wa
Syria.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia Sergei Lavrov ambaye leo anaelekea
Brunei ili kushiriki katika kikao cha jumuiya ya ASEAN, amesema kuwa
Marekani inapaswa kutoa maelezo kuhusiana na kikoa hicho ambacho
kufanyika kwake kulipendekezwa na Moscow pamoja na Washington kwa ajili
ya kutatua mgogoro wa Syria.
Lavrov ameongeza kwamba yeye na mwenzake wa
Marekani walikubaliana kuishawishi serikali ya Syria na waasi
wanaofadhiliwa na nchi za kigeni kutafuta suluhisho la kisiasa la
mgogoro huo.
Katika upande mwingine serikali ya Syria imetangaza kuwa, mapigano ya
miaka mwili yaliyosababishwa na magaidi wanaofadhiliwa na nchi za
kigeni yameharibu majengo 9,000 na kuleta hasara ya dola bilioni 15.







No comments:
Post a Comment