NCHI wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) zinatakiwa kuunganisha nguvu zao kwa pamoja, ili kupambana na fedha haramu na ongezeko la ufadhili wa vitendo vya kigaidi katika kanda hiyo.
Waziri wa Usalama wa Burundi, Gabriel Nizigama alisema hayo jana wakati wa kufungua warsha ya siku nne ya wataalamu fedha haramu na ufadhili wa ugaidi, mjini Bujumbura, Burundi.
‘’Nchi za EAC zinaweza kufanikiwa katika kuzuia na kupambana na fedha haramu na ufadhili wa ugaidi kupitia juhudi za pamoja,’’ alisema.
Waziri wa Usalama wa Burundi, Gabriel Nizigama alisema hayo jana wakati wa kufungua warsha ya siku nne ya wataalamu fedha haramu na ufadhili wa ugaidi, mjini Bujumbura, Burundi.
‘’Nchi za EAC zinaweza kufanikiwa katika kuzuia na kupambana na fedha haramu na ufadhili wa ugaidi kupitia juhudi za pamoja,’’ alisema.





