Wapiganaji wa makundi yanayopigania kujitenga maeneo ya mashariki mwa
Ukraine wamedai kuuzingira mji wa kistratejia wa Debaltseve. Wapiganaji
hao pia wamesema mbali na mji huo, pia wamewazingira wanajeshi zaidi ya
1000 wa Ukraine mjini hapo. Serikali ya Kiev imekanusha madai hayo na
kusema mapigano bado yanaendelea. Mji huo wa Debaltseve una umuhimu
mkubwa kwani ndio unaotumiwa na wanajeshi wa serikali ya Ukraine
kupitishia vifaa muhimu kutoka Kiev.
Hayo yanajiri katika hali ambayo,
kesho marais wa Russia, Ukraine, Ufaransa na Kansela wa Ujerumani
wanatarajiwa kukutana mjini Minsk nchini Belarus ili kujadili namna ya
kuhitimisha mapigano mashariki mwa Ukraine. Nchi za Ulaya zinaituhumu
Russia kuwa inawaunga mkono wanamgambo wanaopigania kujitenga na Ukraine
lakini Moscow imekuwa ikikanusha vikali madai hayo na kuzilaumu nchi za
Ulaya kuwa ndizo zilizopelekea kuzuka machafuko hayo baada ya kuunga
mkono mapinduzi yaliyomuondoa madarakani raia aliyechaguliwa kidemokrasi
nchini humo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment