Rais Bashar al-Assad wa Syria amekataa kushirikiana na muungano wa
Marekani dhidi ya Daesh, kutokana na muungano huo kuendelea kuyaunga
mkono magenge hayo yanayotenda jinai. Amesema kuwa, serikali ya Damascus
haiwezi kushirikiana na nchi hizo ingawa pia amesema kuwa inaweza
kushirikiana na nchi nyengine.
Rais al-Assad ameyasema hayo katika
mahojiano maalumu aliyofanyiwa na televisheni ya BBC na kusisitiza kuwa,
Syria imeshapokea ujumbe kadhaa kutoka muungano huo unaoongozwa na
Marekani ukiitaka nchi hiyo kushirikiana na Washington lakini mara zote
Damascus imekuwa ikikataa ujumbe huo. Amesema na hapa ninamnukuu:
“Tunapinga kuungana na muungano huo kama ambavyo pia hatupendelei
kufanya hivyo. Na sababu iko wazi nayo ni kwamba, hatuwezi kuungana na
nchi ambazo zinaunga mkono ugaidi. Wanakanyaga kanuni wazi wazi, hasa
inapokuwa kadhia ni ya Syria.” Mwisho wa kunukuu. Akielezea madai ya
Marekani ya kuwapatia mafunzo ya kijeshi watenda jinai ikidai kuwa ni
wapinzani wenye misimamo ya wastani, amesisitiza kuwa, madai hayo hayana
ukweli wowote na ni ndoto kwa Damascus kukubali kushiriki kwenye
mungano wa unaoongozwa na Marekani. Aidha Rais Bashar al-Assad amesema
kuwa, aidolojia ya kundi la kitakfiri la Daesh na makundi mengine kama
hilo, ni aidolojia ile ile ya Uwahabi unaoungwa mkono na ukoo wa
Aal-Saudi wa nchini Saudia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment