Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, February 10, 2015

Wahajiri 29 wa Kiafrika wafariki kisiwani Lampedusa

Takriban wahajiri haramu 29 wa Kiafrika wamepoteza maisha katika kisiwa cha Lampedusa karibu na Italia. Habari zinasema kuwa wahajiri wasiopungua 100 wamezuiwa kuingia Ulaya na wanajeshi wa baharini wa Italia ambapo 29 kati yao wamefariki dunia baada ya kupigwa na baridi kali. Baadhi ya wahajiri hao wanaendelea kupata matibabu katika hospitali moja kwenye kisiwa cha Sicily nje kidogo ya Lampedusa.
Hii si mara ya kwanza kwa wahajiri haramu wa Kiafrika kupoteza maisha wakiwa safarini kuelekea Italia. Mwaka uliopita pekee, zaidi ya wahajiri 3200 walipoteza maisha kwenye safari za aina hiyo. Mwaka 2013 wahajiri wa Kiafrika wasiopungua 360 walipoteza maisha baada ya meli yao kuzama katika kisiwa cha Lampedusa. Wengi wa wahajiri hao haramu huwa ni kutoka nchi zilizoko chini ya jangwa la Sahara.

No comments: