Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, February 10, 2015

Seleka wakabiliana na askari wa UN huko CAR

Maeneo kadhaa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati yameshuhudia mapigano kati ya askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa na muungano wa zamani wa waasi wa Seleka. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na askari hao wa Umoja wa Mataifa, mapigano hayo yalijiri katika eneo la Bria, katikati mwa nchi hiyo.
Inaelezwa kuwa, mapigano hayo makali kati ya pande mbili yaliibuka baada ya askari wa Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na askari wa Ufaransa, kutaka kuwapokonya waasi hao wa Seleka majengo ya serikali ambayo wamekuwa wanadhibiti kwa muda mrefu sasa, suala ambalo limezusha mapigano makali. Hata hivyo taarifa kamili ya idadi ya watu waliouawa au kujeruhiwa bado haijatolewa. Mbali na waasi wa Seleka, askari hao wa kusimamia amani wa Umoja wa Mataifa, wamekuwa wakikabiliwa pia na mashambulizi kutoka kwa wanamgambo wa kundi la kigaidi la Anti-Balaka suala ambalo wiki kadhaa zilizopita, lilipelekea askari kadhaa wa umoja huo kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa. Jamhuri ya Afrika ya Kati ilitumbukia katika mapigano makali ya kikaumu hapo mwaka 2013 na kupelekea maelfu ya watu kuuawa, wengi wao wakiwa ni Waislamu.

No comments: