Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Admeli
Habibullah Sayyari amesema kuwa, karibuni hivi jeshi la wanamaji la Iran
litazindua meli ya kisasa aina ya Damavand ambayo imeundwa na wataalamu
wa hapa nchini. Akiashiria uwezo wa jeshi la Iran katika kujibu
chokochoko zozote za adui katika sherehe za kuadhimisha kumbukumbu ya
Mapinduzi ya Kiislamu ya nchini Iran, Kamanda Habibullah Sayyari amesema
kuwa, hii leo taifa la Iran linajivunia juhudi za wasomi na vijana wake
ambao wameweza kuzalisha aina mbalimbali ya silaha na zana za kisasa
kabisa kwa kiwango cha kimataifa.
Ameyataja mafanikio hayo kuwa ni mwiba
kwenye macho ya maadui wasiolitakia mema taifa na watu wa Iran ya
Kiislamu. Aidha ameelezea matatizo yaliyokuwa yakilikabili jeshi la Iran
katika kipindi cha utawala wa Shah kutokana na kufuata kibubusa siasa
za Marekani na kuongeza kuwa, wakati ule maamuzi na mipango yote
yaliyokuwa yakihusu zana, silaha, mazoezi ya kijeshi na mambo mengine
yalikuwa yakichukuliwa na Washington bila ya kuwahusisha wataalamu wa
Iran, suala ambalo liliifanya Iran kubakia tegemezi wakati wote. Amesema
kuwa, tangu mwanzoni mwa vita vya kulazimishwa vya miaka minane, Imam
Khomein (MA) alitoa somo kwa jeshi la Iran kujiamini, jambo lililoifanya
Iran iweze kusimama kidete dhidi ya mabeberu kwa uwezo wa Mwenyezi
Mungu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment