Naibu Mkuu wa Mkoa wa Imran nchini Yemen amesema kuwa watu zaidi ya 100
wameuawa katika mapigano yaliyozuka baina ya jeshi la serikali na
wapiganaji wa al-Huthi kaskazini mwa nchi hiyo. Ahmad al-bakri, amesema
kuwa, mapigano makali yamejiri kati ya pande mbili ambapo karibu watu
120 wameuawa. Kwa mujibu wa afisa huyo wa serikali, watu 100 kati ya
wahanga hao ni wapiganaji wa al-Huthi na kwamba 20 wengine ni askari wa
serikali.
Hii ni katika hali ambayo Brigedia Jenerali Ahmad Ali
al-Ashul, wa jeshi la Yemen, amezilaumu baadhi ya pande ambazo
hakuzitaja, kwamba zinafanya njama kwa lengo la kuzusha vita vya ndani
nchini Yemen na kusisitiza kuwa, njama hizo zitaambulia patupu.
Wanachama wa al-Huthi wanaituhumu serikali ya Sanaa kuwa inayaunga mkono
makundi ya kitakfiri huko kaskazini mwa nchi hiyo kwa lengo la
kudhoofisha nafasi yao, sambamba na kuandaa mazingira ya kupenya
matakfiri katika mkoa huo wa Imran wa kaskazini mwa Yemen.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment