Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 3, 2014

'Wasyria wataamua hatima yao katika uchaguzi wa rais'

Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria Walid al Muallem, amesema kuwa irada ya wananchi wa Syria ndiyo pekee itakayoweza kuainisha mustakbali wa nchi hiyo. Al Muallem ameyasema hayo leo baada ya kushiriki katika uchaguzi wa rais wa nchi hiyo na kuongeza kuwa, kujitokeza kwa wingi sana wananchi katika uchaguzi wa leo wa kidemokrasia na huru, kutaainisha mustakbali wa taifa hilo.
Amesema, Wasyria wameshiriki katika uchaguzi huo kwa uhuru na kwamba, serikali ya Damascus inawapa umuhimu mkubwa wananchi kwani ni wananchi hao ndio wenye haki ya kuchagua mfumo wanaoutaka. Amesisitiza kuwa, hivi karibuni ulimwengu utashuhudia kushindwa njama za maadui wa taifa hilo. Ameusifu ushiriki mkubwa wa wananchi katika uchaguzi wa leo na kusema kuwa, uchaguzi huo utaandaa mazingira ya amani, utulivu, ujenzi mpya wa nchi na kutatuliwa kisiasa mgogoro wa nchi hiyo ya Kiarabu. Kwa upande mwingine amekusifu kusimama kidete na muqawama wa taifa hilo dhidi ya njama na hila za maadui wasioitakia mema Syria. Rais Bashar al-Assad wa Syria amepiga kura katika kituo cha kupigia kura cha eneo la Hayyu al-Maliki mjini Damascus, huku Hassan Abdullah al Nouri, mgombea mwengine wa nafasi hiyo akipiga kura katika moja ya vituo vilivyowekwa katika hoteli ya Sheraton mjini Damascus, ambapo pamoja na mambo mengine alisisitiza kuwa, uchaguzi huo ni wa kidemokrasia na huru. Zaidi ya watu milioni 15 waliotimiza masharti ya kupiga kura wameshiriki kwa katika uchaguzi  wa leo. Wakati huo huo Spika wa bunge la Syria, Mohammad Jihad Al-Liham, amesema kuwa, ushiriki mkubwa wa Wasyria katika uchaguzi wa leo umewashangaza walimwengu. Uchaguzi wa rais nchini Syria umefanyika katika mikoa yote ya nchi hiyo, ispokuwa mkoa wa al-Riqqah ambao unadhibitiwa na magenge ya kigaidi.

No comments: